Muendelezo:
UZAZI WA MPANGO KWA MTU ALIYETOKA KUTOA MIMBA AU MIMBA KUTOKA AU KUHARIBIKA..
kwanza unatakiwa kujua kuwa ni miiko ya kimaadili kwa daktari kujudge kuwa huyu mtu katoa mimba, kama kakosea au hamna sio kazi yake na wala hawezi kukuuliza wewe ukifika mwambie umetoa mimba unataka huduma atakuhudumia kama mtu au mgonjwa mwingine yeyote... pia ni kosa kisheria na kimaadili kushare taarifa za mgonjwa na hivyo ni sahihi nikisema kama ukiwa na miaka 16 na kuendelea siri zako hata mzazi wako hatajua ili mradi hutaki ajue.. hatutakiwi kureport kwenye vyombo vya dola ikiwa mtu kaja hospitali na katoa mimba kuomba msaada atajuana na mungu wake isipokuwa kama kuna kiasi kikubwa cha utoaji wa mimba katika jamii fulani daktari anawajibika kutoa taarifa ili elimu itolewe na pia hatatoa majina ya waliotoa mimba.. pia kuna sheria inayomzuia dr. Kutoa mimba ambayo haihatarishi uhai wa mama mjamzito japo kwa nchi nyingine kama ethiopia zambia south africa na nchi nyingi za magharibi wanasheria inayoruhusu kutoa mimba kama mtu kabakwa au anajua hawezi kutake care of the family. Najadili hili kwa sababu nimekutana na mabinti au wadada wengi wametoa mimba lakini wanaogopa kwenda hospitali mpaka wakati mwingine wanaogopa hata wanaombwa rushwa pengine au wanatumia gharama kubwa kusafishwa kwenye hospitali za binafsi na huku ni huduma ambayo wangepewa hospitali za serikali kama mgonjwa mwingine yeyote na kama una bima hulipi chochote.
Nachochea utoaji mimba?? I dont know... i dont support abotion but sitaki mtu afe au apate shida baada ya kutoa mimba kitu ambacho kinazuilika
Back to the topic...
Mwanamke baada ya mimba kutoka huwa anaweza kurudi kwenye mzunguko wake wa kawaida maana yake yai kutoka baada ya siku 14 hivyo sio lazima uone siku zako kwanza ndio useme upo katika hatari ya kupata ujauzito... kwa sababu yai linatoka kwanza ndio hedhi baadae inatoka.. hivyo unaweza kupata mimba na huku bado hujaona siku zako..ndio maana nilikuwa nasisitiza kutymia uzazi wa mpango au kuacha kufanya mapenzi kabla ya angalau wiki 6 miezi mitatu mpaka 6 ndio upate ujauzito
Be healthy and happy
I love medicine i love humanity
@ dr.ibu
Acha maoni ako hapo chini pia unaweza kutuma swali lako kupitia whatsap no 076757271 jina lako litakua siri
kujiunga na group la whatsap bonyeza hapo https://chat.whatsapp.com/3fsRnLDkTZIFMqasAjJXWU
Be healthy and happy
3 comments:
Mbona no haipo WhatsuApp jomonš
Mbona namba ziko 9?
Vp kuus wiki 3
Post a Comment