Monday, 15 October 2018

Mpenzi wangu ana ugonjwa wa sickle cell anatumia dawa naombeni ushauri

Topic.For istance ulikuwa na mpenz na mnapendana saana toka upo fom four ye akiwa fom two, mkaishi vizuri   kwa upendo na kwa ahati kuwa mtakuja kuoana.

Mkakua wew ukapanda advanc asichana akamaliza fom four lenu bado ni moja, msichana anaheshima sana, anawaheshimu ndg zako alafu mcha mungu.

Baada ya kumaliza six huku mkiendelea kuwasiliana ukachuguliwa chuo kikuu nayeye Advance... Baadae ukiwa mwaka wa tatu yeye akanza kusoma chuo mwaka wa kwanza.

Mkaamua awe anakuja kutembea mnaonana maana mmoja Muhimbili mwingine Udsm lakin baadae akija akawa anameza dawa za kuongeza dam baada ya kumuhoji vizur akasema anatatizo la dam tuu.
Ukaanza kufuatilia kwa rafik zake ukaja kuambia hua anaishiwa dam mara kwa mara na kuishiwa nguvu Yan kumbe ana sikle cell

Utachukua uamuz gan yeye anasikle cell isiyo na dalili za nje utamuacha au?? NAOMBEN USHAURI

Ushauri : kabla ya kukupa ushauri yafaa ukaujua ugonjwa kwanza ili ikusaidie kuamua na ndio jukumu langu kama daktari.Okey actually sickle cell ni seli mundu kwa kiswahili.. ni hali tu ambayo umbo la seli hai nyekundu  za damu linakuwa kama mwezi mchanga au mundu au sickle ile ya kukatia majani ya ng'ombe ndio jina lilikotoka... seli hai nyekundu za damu ndio seli zinazohusiana na kusafirisha hewa ndani ya mwili wa binadamu. Kawaida huwa zinakuwa na umbo la duara liliobonyea katikati kama disc. Ambapo watu wenye sickle cell wanakuwa na tofauti hiyo. Huu ni ugonjwa  wa kurithi ambao lazima urithi kwa wazazi wote wawili baba na mama. Baba na mama wanaweza wakawa na vinasaba  vya sickle cell lakini hawana ugonjwa AS(heterozygous )  lakini wana hatari ya kuzaa mtoto mwenye sickle SS cell kwa uwezekano wa 25?  Ila kama mmoja wa wazazi ana ugonjwa wa sickle cell SS na baba yuko kawaida hana hata vinasaba AA watazaa watoto wenye vinasaba lakini hawana ugonjwa wa sickle cell AS. Kumbukumbu ya genetics kidogo...
Watu wenye sickle cell wanaishi kama watu wengine tu na wengine hugundulika ukubwani hadi miaka ya 40?
Matatizo wanayopata watu wenye sickle cell..
Mara nyingi matatizo wanayopata yanatokana na ile shape ya hizo seli hai nyekundu...
Kwa seli zilivyo haziwezi kudumu muda mrefu kama  seli hai nyekundu za kawaida... seli hai nyekundu zinaishi siku 120 lakini zenye sickle cell zinaishi siku hadi 15 tu. Hivyo mtu huyu atakuwa na upungufu wa damu wa kudumu. Mtu wa kawaida damu yake hb ni 11 hadi 17 lakini kwa hawa watu wanakuwa na damu mpaka 6 au 7 na huwa hazifanani wengine 8, 9 ,10 na wengine kawaida..kwa hiyo huwa tunawapa dawa za kuongeza damu kila siku kidonge kimoja cha folic acid.
Itaendelea
Dr.ibu 
Acha maoni ako hapo chini pia unaweza kutuma swali lako kupitia whatsap no 076757271 jina lako litakua siri kujiunga na group la whatsap bonyeza hapo https://chat.whatsapp.com/3fsRnLDkTZIFMqasAjJXWU Be healthy and happy

No comments: