Wednesday, 17 October 2018

"UKIBAKWA USIOGE, KUNYOA NYWELE WALA KUKATA KUCHA" DR.IBU

USHAHIDI WA KITAALAMU KWA ALIYEBAKWA.

ushahidi wa kitaalamu kwa aliyebakwa kuhusiana na mtuhumiwa aliyembaka unakusanywa na daktari kujua endapo  ni kweli mtu huyu kabakwa au sio kweli.
Ili kujua kuwa ni kweli mtu kabakwa au hamna hasa kwa wanawake basi kuna vitu vingi.
1. Uwepo wa michubuko sehemu za siri nje au ndani ya uke.
Ikumbukwe kuwa mtu anayebakwa mara nyingi haandaliwi kihisia kwa hiyo ni rahisi kuchubuka na pia sehemu ya nje ya uke mf.mashavu na kinena huwa kinavimba kwa kuumizwa.

2.uwepo wa shahawa ndani ya uke.
Hii inaweza kutumika endapo kosa hili limetendeka ndani ya siku 3 za mwanzoni lakini ina mapungufu mengi mfano:

 a) kuna watu wanamwaga majimaji ambayo hayana mbegu za kiume kwa hiyo hautakuta kitu au ni chache sana kwahiyo ndani ya masaa kadhaa hutakuta mbegu yoyote ilobakia.

b) kuna watu wamekata mirija inayoleta mbegu za kiume kwenye uume kama njia ya uzazi wa mpango ko wao hawatoi mbegu wanatoa majimaji tu.

c) kuna watu wengi hasa wazee ambao walishakuwa na kansa ya tezi dume wanafanyiwa upasuaji wa kutoa korodani zote mbili na hivyo hawawezi kutoa mbegu za kiume.

d)kuchelewa kufika kituo cha huduma ndani ya huo muda.

e) matumizi ya kinga kama kondomu na dawa za kuulia mbegu (spermicide)

MHUSIKA ATATHIBITISHWAJE

kwa kutumia DNA inayoweza kupatikana kwenye vyanzo mbalimbali kama nywele za sehemu za siri, shahawa,pamoja na mabaki yanayopatikana kwenye kucha za mwanamke katika harakati za kujinasua, mara nyingi wanawake hutumia kama silaha hata kama ni fupi lakini sampuli inayotakiwa ni kidogo sana kwahiyo usipuuze.

KAZI YA DAKTARI AU MHUDUMU WA AFYA

a)kumhudumia mgonjwa aliyepata na tukio hilo kwa usiri na kutotangaza

b) kukusanya na kutunza ushahidi wote kwa sababu hii ni kosa la kisheria

C) kutoa ushahidi wa kitaalamu mahakamani kwa maandishi

d) kushauri kuripoti katika vyombo vya dola kuhusiana na matukio ya aina hii.

HUDUMA ZA KIAFYA ZINAZOTOLEWA KWA MTU ALIYEBAKWA.
1. Kutibu majeraha kama michubuko na vidonda
2.kumsaidia kisaikolojia kumuondolea msongo wa mawazo na ikiwezekana kumpa dawa zitakazosaidia kuondoa woga na msongo wa mawazo na kumchunguza kama yupo katika hatari ya kujiua.

3.kuzuia mimba. Akipimwa akikutwa hana mimba ndio anapewa njia za kuzia mimba ila kama anayo anakuwa aliipata kabla ya kubakwa.Hapa inategemea kaja siku ngapi baada ya kubakwa. Akija ndani ya masaa 72 au siku tatu anapata P2 kuzuia mimba akija kuanzia siku 4 mpaka 10 anapewa loop (kitanzi). Akija baada ya hapo kwa nchi nyingine anapimwa akiwa mjamzito mimba inatolewa. Kwetu sheria ya kutoa mimba hairuhusu hiki kipengele bado.

4. Kuzuia magonjwa ya ngono
Atapewa antibiotics kuzuia magonjwa kama gonorrhea kaswende na klamidia.

5. Kuzuia maambukizi ya virusi vya UKIMWI, kwanza mtu huyo atapimwa kwanza akikutwa na maambukizi maana yake alishakuwa amepata kabla ya kubakwa kwa hiyo atapelekwa CTC kuanza matibabu kwa sababu kipimo hakiwezi kusoma maambukizi uliyoyapata kwa muda mfupi kiasi hicho. Kama hana maambukizi anapewa dawa ya kuzuia kuambukiwa kwa sababu hatujui aliyembaka alikuwa ameathirika au alikuwa mzima. Atatumia kwa siku 28 alafu atapimwa tena.
NAMNA GANI YA KUTUNZA USHAHIDI NA KUFANYA MTU AKIBAKWA.
1. Kuwahi mapema hospitali hii itasaidia kupata ushahidi wa kutosha, kuzuia mimba, magonjwa ya zinaa pamoja na UKIMWI
2.usioge au kujisafisha kwa njia yoyote ile
3.usibadilishe nguo au ukibadilisha fika nazo ulizovaa hospitali zihifadhiwe
4.usinyoe
5. Sema na watu jieleze usiogope usije ukapata msongo wa mawazo ambao unaweza kupelekea kujiua.

Mwandishi Dr.ibu.

Acha maoni ako hapo chini pia unaweza kutuma swali lako kupitia whatsap no 076757271 jina lako litakua siri kujiunga na group la whatsap bonyeza hapo https://chat.whatsapp.com/3fsRnLDkTZIFMqasAjJXWU Be healthy and happy

KIPIMO CHA KAMERA KUANGALIA NJIA KUBWA KINAFANYIKAJE?

SWALI; Daktari samahani nataka kujua, mdogo wangu anaumwa yupo hospitali, ugonjwa wake ni anapungukiwa damu mara kwa mara na hata akiongezewa inakaa kidogo anaongezwa tena. damu yake ni kundi O negative kwa hiyo ni taabu kupatikana. madaktari wamesema kesho anafanyiwa kipimo cha kuingiza kamera kwenye njia ya haja kubwa nina hofu sijui kinafanyikaje na madhara yake ni yapi?



JIBU: pole sana kwa familia na mgonjwa na pili nashukuru kwa kuleta swali lako ili pia wengine wajifunze...ni kweli damu group O negative ni ya watu wachache zaidina mbaya zaidi ni kwamba ni lazima ampate mwenye group O negative mwenzake ndipo anaweza kuongezewa damu. kuna vyama kabisa vya watu wenye damu group hilo sehemu nyingi dniani ili kusaidiana endapo mmoja akiwa anhitaji msaada wa damu. bahati mbaya hapa kwetu utaratibu huu haupo. Pia uhitaji wa damu ya kundi hili ni mkubwa kwa sababu hutumika zaidi mazingira ya wagonjwa wa dharura EMERGENCY DEPARTMENTS duniani kote kwa sababu unawza kumuongezea mtu yeyote hata kama hujui kundi lake a damu au huna mashine au muda wa kupima kundi lake la damu.

Tukirudi kwenye hiyo kipimo anachofanyiwa ndugu huyu kinaitwa colonoscopy. Hiki ni kifaa cha kisasa kabisa kinachotumika kuangalia utumbo mkubwa kama kuna vidonda au uvimbe au michubuko na kansa ya utumbo mkubwa. Kinatokana  na neno colon likimaanisha utumbo mkuwa na scopy nikuangalia. Hospitali kubwa hizi kama BUGANDO na MUHIMBILI na nyinginezo zinacho hichi kipimo.
Image
Mara nyingi watu wanafanyiwa colonoscopy wazee ili kuangalia kansa ya utumbo kuanzia miaka a 50 na kuendelea, inaweza kutumika kama njia ya uchunguzi tu mtu akiwa hana dalili kitaalamu tunaita screening ili kuiwahi kansa kabla haijasambaa, pia inatumika kuangalia ugonjwa unaitwa polyp ambazo ni uvimbe ambao unakuwa mithili ya vidole unakuwa kwenye utumbo na ni ugonjwa wa kurithi na ina nyingine za polyp hizi huwa zinakuja kubadilika na kuleta kansa au saratani. Kama mgonjwa akiwa na polyp kwa kutumia hiki kifaa daktari anaweza akazitoa wakati wa kufanya kipimo kitu ambacho kitapunguza uwezekano wa kupata kansa..
kuna njia nyingi za kugundua kama kuna kansa lakini waliowengi tunaona njia hii inakuwa rahisi zaidi kwa sababu inatoa uhuru wa kuona na kufanya matibabu kama kuchukua sampuli biopsy na kutibu kama kutoa polyp
Je kila mtu aende akafanyiwe colonoscopy? 
Tunashauri watu wafanye kama njia ya kuangalia kama wana magonjwa kama kansa ya utumbo mkubwa colonic cancer wakiwa na umri wa miaka 50 na kuendelea. Pia baadhi ya watu ambao wapo katika hatari ya kupata kansa ya utumbo mkubwa kama ambao katika familia kunamtu alishawahi pata huu ugonjwa kwa sababu huwa unarithishwa ko hawa wanaweza wakaanza wakiwa na umri mdogo hata 20.
sababu gani daktari ataamua kukufania colonoscopy?
kukiwa na damu kwenye kinyesi au kutoa tu dmu kwenye njia ya haja kubwa
kama utoaji choo wako unabadilika mara unaharisha unapata choo kigumu...yaani inabadilika kutoka ile kawaida yako
kupungukiwa damu mara kwa mara bila sababu inayojulikana mf. hujapata ajali 
Tumbo kuvimba au kuuma mud mrefu bila sababu ya msingi
kuhisi kama unajisikia haja imekubana na ukienda chooni unahisi kinyesi kimebakia ndani hakijaisha 
kama ulishawahi kuwa na kansa kabla au polyp kabla

Nini cha kufanya kabla ya colonoscopy? 
     Utaambiwa vyakula ambavyo unatakiwa kula na ambavyo hutakiwi kula. Mara nyingi nawaambia wagonjwa wale vyakula ambavyo hakiai sana tumboni wasile vyakula vyenye mafuta sana na mara nyingi wanywe maji ya kutosha na vyakula vyenye nyuzi nyuzi kama mboga majani na matunda siku moja kabla. Kuna dawa kama ulikuwa unazitumia unaweza kuzuliwa kutumia kwa sababu zitakuwa na muingiliano na kipimo. na utapewa karatasi yenye maelezo.Utumbo wote huwa unasafishwa kabla ya kufanya kipimo hiki ili kamera iweze kupita na daktari aweze kuona. hivyo utapea dawa ambayo itasafishautumbo na utaharisha kila kitu kitoke na inatakiwa unywe dawa yote utakayopewa na ni vizuri kumwambia daktari kama una hofu au shida yoyote katka maandalizi haya ili usiende kinyume.Kinavyofanyika kipimo hiki unapewa dawa ya usingizi ili uwe na amani na urelax na usiwe na maumivu, kisha inaingizwa kama kityubu ambacho kinakuwa na kamera kwa mbele na kisha unawashwa mwanga ndio daktari anakuwa anaona kwenye screen 
baada ya kipimo hiki unaweza kuendelea kula kama kawaida siku hiyo hiyo ila tunashauri usifanye kazi au kukaa sana unatakiwa kupumzika na utaanza kutumia dawa zako ambazo labda uliziacha ili kupisha kipimo.
ukiona yafuatayo unaweza kwenda hospitali baada ya colonoscopy.
kutapika
tumbo kuwa na maumivu makali
tumbo kuvimba na kuwa gumu au kujaa 
kutoka damu nyingi sehemu ya haja kubwa
kupata homa kali au kucemka mwili

Be healthy and happy


Acha maoni ako hapo chini pia unaweza kutuma swali lako kupitia whatsap no 076757271 jina lako litakua siri kujiunga na group la whatsap bonyeza hapo https://chat.whatsapp.com/3fsRnLDkTZIFMqasAjJXWU

Nini husababisha majimaji na harufu kwenye uke?

MAJIMAJI NA HARUFU KWENYE UKE

Ute kwenye uke ni nini? — hili ni neno ambalo hutumika na wataalamu wa afya kuelezea maji maji yanayokuwa au kutoka katika sehemu za siri za mwanamke au uke"Vaginal discharge"
 Maji maji haya ni muunganiko wa seli za mwili hasa za kuta za uke na shingo ya kizazi pamoja na bakteria ambao huishi kwenye uke.

Je hii hali inaweza kuwa ya kawaida? — Ndio kwa mwanamke ambaye hana tatizo lolote maana yake anapata hedhi ya kawaida  huwa anakuwa na ute huu au majimaji haya lakini ni kiasi kidogo
Kwa kawaida ute au majimaji haya huwa ni meupe au clear kama maji au mazito mazito ila huwa hayatoi harufu yoyote.
Wanawake wanatofautiana
Katika kiasi cha majimaji ambayo huwa yanakuwa kwenye uke wengine huwa wanakuwa na kiasi kikubwa wengine kidogo sana.
Pia mwanamke mmoja anaweza akawa na kipindi kingine anakuwa na majimaji mengi na wakati mwingine kidogo.
Mf. Mwanamke anakuwa na maji mengi zaidi:

●akiwa mjamzito

●akitumia dawa za uzazi wa mpango

●wiki mbili kabla hajaanza period. Ni kipindi yai linatoka kwenye ovari

Pia wanawake ambao wamefika umri wa kutoona siku zao( menopause) huwa wanakuwa na ute kidogo au uke unakuwa mkavu kabisa.

Je majimaji kwenye Uke yanaweza kuwa ni ugonjwa?

NDIO... majimaji kwenye uke yanaweza kuwa ni ugonjwa endapo yataambatana na vitu vifuatavyo:

●muwasho sehemu za siri

●wekundu, maumivu au uvimbe sehemu za siri

●majimaji ambayo ni ya njano au kijani au yanachanganyikana na damu

●majimaji yakiwa yanatoa harufu kali

●kupata maumivu unapokojoa au unapojamiiana

●kupata maumivu chini ya kitovu

●joto kupanda au kuchemka mwili(homa)

NINI HUSABABISHA MAJIMAJI KUTOKA KWENYE UKE KAMA UGONJWA:
Visababishi ni vingi sana ila mara nyingi ni




●mambukizi kwenye uke

Kuacha vitu kwenye uke kama pad au condom

● kutumia sabuni au vitu kemikali nyingine kwenye uke


●homoni kutobalance


NoTE. Ukiona dalili kama hizi usikimbilie kununua dawa na kumeza kwa sababu vyanzo ni vingi nenda hospitali kamuone daktari wako mueleze.
 Daktari atachukua majimaji haya atayapima na kugundua chanzo na utapata dawa kutokana na chanzo cha tatizo..usitumie mitishamba ya insta tatizo linaweza kuzidi kuwa kubwa. Hakuna upasuaji.

Kama majimaji haya yanatokana na maambukizi ya ugonjwa fulani nashauri usifanye mapenzi pia ni vizuri kquongea na mwenzi wako mtibiwe pamoja..

Acha kufanya mapenzi ukiwa unatoa majimaji ambayo sio ya kawaida au yanatoa harufu mpaka ujue kuwa hauna maambukizi ya ugonjwa .

NAMNA YA KUZUIA KUTOKA MAJIMAJI KWENYE UKE AMBAYO SIO YA KAWAIDA AU YENYE KUTOA HARUFU

●Tumia maji ya uvuguvugu
Na sabuni ambayo haitoi harufu yoyote kuosha sehemu zako za siri.sehemu ya juu ya uke

●kuoga maji ya uvuguvugu na usitumie sabuni ambazo zina harufu

.Usitumie spray au poda au perfume kwenye sehemu za siri


●usiingize kitu chochote iwe kidole au kusafisha ndani ya uke kwa njia yoyote ile wala usiingize maji kwenye uke

●baada ya kumaliza haja chooni usitumie karatasi toilet paper zenye harufu au manukato yoyote.

TIBA
Majimaji au harufu kwenye uke inatibiwa kutokana na kisababishi  ambacho hupatikana baada ya kuchukua majimaji haya na kuyapeleka maabara kisha kujua chanzo hasa na mdudu hasa aliyesababisha ndipo utapewa dawa.

Itaendelea
Acha maoni ako hapo chini pia unaweza kutuma swali lako kupitia whatsap no 076757271 jina lako litakua siri kujiunga na group la whatsap bonyeza hapo https://chat.whatsapp.com/3fsRnLDkTZIFMqasAjJXWU Be healthy and happy

Monday, 15 October 2018

Lini naruhusiwa kufanya mapenzi baada ya mimba kuharibika au baada ya kujifungua

Muendelezo:
UZAZI WA MPANGO KWA MTU ALIYETOKA KUTOA MIMBA AU MIMBA KUTOKA AU KUHARIBIKA..
kwanza unatakiwa kujua kuwa ni miiko ya kimaadili kwa daktari kujudge kuwa huyu mtu katoa mimba, kama kakosea au hamna sio kazi yake na wala hawezi kukuuliza wewe ukifika mwambie umetoa mimba unataka huduma atakuhudumia kama mtu au mgonjwa mwingine yeyote... pia ni kosa kisheria na kimaadili kushare taarifa za mgonjwa na hivyo ni sahihi nikisema kama ukiwa na miaka 16 na kuendelea siri zako hata mzazi wako hatajua ili mradi hutaki ajue.. hatutakiwi kureport kwenye vyombo vya dola ikiwa mtu kaja hospitali na katoa mimba kuomba msaada atajuana na mungu wake isipokuwa kama kuna kiasi kikubwa cha utoaji wa mimba katika jamii fulani daktari anawajibika kutoa taarifa ili elimu itolewe na pia hatatoa majina ya waliotoa mimba.. pia kuna sheria inayomzuia dr. Kutoa mimba ambayo haihatarishi uhai wa mama mjamzito japo kwa nchi nyingine kama ethiopia zambia south africa na nchi nyingi za magharibi wanasheria inayoruhusu kutoa mimba kama mtu kabakwa au anajua hawezi kutake care of the family. Najadili hili kwa sababu nimekutana na mabinti au wadada wengi wametoa mimba lakini wanaogopa kwenda hospitali mpaka wakati mwingine wanaogopa hata wanaombwa rushwa pengine au wanatumia gharama kubwa kusafishwa kwenye hospitali za binafsi na huku ni huduma ambayo wangepewa hospitali za serikali kama mgonjwa mwingine yeyote na kama una bima hulipi chochote.

Nachochea utoaji mimba?? I dont know... i dont support abotion but sitaki mtu afe au apate shida baada ya kutoa mimba kitu ambacho kinazuilika

Back to the topic...

Mwanamke baada ya mimba kutoka huwa anaweza kurudi kwenye mzunguko wake wa kawaida maana yake yai kutoka baada ya siku 14 hivyo sio lazima uone siku zako kwanza ndio useme upo katika hatari ya kupata ujauzito... kwa sababu yai linatoka kwanza ndio hedhi baadae inatoka.. hivyo unaweza kupata mimba na huku bado hujaona siku zako..ndio maana nilikuwa nasisitiza kutymia uzazi wa mpango au kuacha kufanya mapenzi kabla ya angalau wiki 6 miezi mitatu mpaka 6 ndio upate ujauzito

Be healthy and happy
 I love medicine  i love humanity
@ dr.ibu
Acha maoni ako hapo chini pia unaweza kutuma swali lako kupitia whatsap no 076757271 jina lako litakua siri kujiunga na group la whatsap bonyeza hapo https://chat.whatsapp.com/3fsRnLDkTZIFMqasAjJXWU Be healthy and happy

Nini cha kufanya mimba ikitoka??

NINI CHA KUFANYA MIMBA IKITOKA AU BAADA YA KUTOA MIMBA..

Baada ya mimba kutoka au mimba ikitoka kutokana na sababu mbalimbali iwe umekunywa dawa bila kujua au kwa kujua zikasababisha mimba kutoka basi kuna vitu vingi ambavyo unatakiwa kuzingatia...kwanza kama ndio umeona damu tu imetoka nenda hospitali  mara moja kwa sababu damu ikitoka sana inasababisha upungufu wa damu na moyo huwa unaweza kufeli... pia unatakiwa kuhakikisha hakuna mabaki ya kiumbe au masalia ya damu yanayobaki kwenye mfuko wa uzazi na njia pekee ni kwenda hospitali kusafishwa kizazi.. lakini pia unatakiwa kupewa dawa za kuzuia maambukizi ya bacteria.. hii ni kutokana na kwamba mlango wa shingo ya kizazi upo wazi baada ya mimba kutoka hivyo inakuwa kwenye hatari ya kupata infection....ko unapata antibiotics angalau siku 7 mpaka 10.... tatu ni kutafuta chanzo cha mimba kutoka kama mimba imetoka inaweza sababu iliyosababisha mimba moja kutoka ikasababisha mimba inayofuata pia ikatoka... hivyo ni vizuri kutafuta chanzo ili kutibiwa kabla ya kupata mimba nyingine..
Nne ni uzazi wa mpango..
Ni rahisi zaidi mtu kupata mimba baada ya mimba kutoka pindi tu atakapofanya mapenzi...
Hivyo sio lazima aanze kupata mzunguko wake ndio awe katika hatari ya kupata ujauzito. Hatari yake ni kuwa chanzo chake cha mimba kutoka kinaweza kusababisha mimba kutoka tena na pia via vyake vya uzazi vinakuwa havijatengamaa kupata nguvu ya kubeba mimba tena kitu ambacho ni hatari kwa mama na mtoto aliyepo tumboni... hivyo tunashauri mama asijihusishe na kufanya mapenzi baada ya mimba kutoka au kuzaa mpaka siku 42 zitimie wiki 6 au mwezi mmoja na wiki mbili... lakini tunashauri aipate mimba mpaka angalau miezi mitatu mpaka sita baada ya kupoteza mimba...

Nini madhara ya kufanya mapenzi mapema mara tu baada ya mimba kutoka au kuzaa.?
See me at www.ibumd.blogspot.com kwa muendelezo
Acha maoni ako hapo chini pia unaweza kutuma swali lako kupitia whatsap no 076757271 jina lako litakua siri kujiunga na group la whatsap bonyeza hapo https://chat.whatsapp.com/3fsRnLDkTZIFMqasAjJXWU Be healthy and happy

Mpenzi wangu ana ugonjwa wa sickle cell anatumia dawa naombeni ushauri

Topic.For istance ulikuwa na mpenz na mnapendana saana toka upo fom four ye akiwa fom two, mkaishi vizuri   kwa upendo na kwa ahati kuwa mtakuja kuoana.

Mkakua wew ukapanda advanc asichana akamaliza fom four lenu bado ni moja, msichana anaheshima sana, anawaheshimu ndg zako alafu mcha mungu.

Baada ya kumaliza six huku mkiendelea kuwasiliana ukachuguliwa chuo kikuu nayeye Advance... Baadae ukiwa mwaka wa tatu yeye akanza kusoma chuo mwaka wa kwanza.

Mkaamua awe anakuja kutembea mnaonana maana mmoja Muhimbili mwingine Udsm lakin baadae akija akawa anameza dawa za kuongeza dam baada ya kumuhoji vizur akasema anatatizo la dam tuu.
Ukaanza kufuatilia kwa rafik zake ukaja kuambia hua anaishiwa dam mara kwa mara na kuishiwa nguvu Yan kumbe ana sikle cell

Utachukua uamuz gan yeye anasikle cell isiyo na dalili za nje utamuacha au?? NAOMBEN USHAURI

Ushauri : kabla ya kukupa ushauri yafaa ukaujua ugonjwa kwanza ili ikusaidie kuamua na ndio jukumu langu kama daktari.Okey actually sickle cell ni seli mundu kwa kiswahili.. ni hali tu ambayo umbo la seli hai nyekundu  za damu linakuwa kama mwezi mchanga au mundu au sickle ile ya kukatia majani ya ng'ombe ndio jina lilikotoka... seli hai nyekundu za damu ndio seli zinazohusiana na kusafirisha hewa ndani ya mwili wa binadamu. Kawaida huwa zinakuwa na umbo la duara liliobonyea katikati kama disc. Ambapo watu wenye sickle cell wanakuwa na tofauti hiyo. Huu ni ugonjwa  wa kurithi ambao lazima urithi kwa wazazi wote wawili baba na mama. Baba na mama wanaweza wakawa na vinasaba  vya sickle cell lakini hawana ugonjwa AS(heterozygous )  lakini wana hatari ya kuzaa mtoto mwenye sickle SS cell kwa uwezekano wa 25?  Ila kama mmoja wa wazazi ana ugonjwa wa sickle cell SS na baba yuko kawaida hana hata vinasaba AA watazaa watoto wenye vinasaba lakini hawana ugonjwa wa sickle cell AS. Kumbukumbu ya genetics kidogo...
Watu wenye sickle cell wanaishi kama watu wengine tu na wengine hugundulika ukubwani hadi miaka ya 40?
Matatizo wanayopata watu wenye sickle cell..
Mara nyingi matatizo wanayopata yanatokana na ile shape ya hizo seli hai nyekundu...
Kwa seli zilivyo haziwezi kudumu muda mrefu kama  seli hai nyekundu za kawaida... seli hai nyekundu zinaishi siku 120 lakini zenye sickle cell zinaishi siku hadi 15 tu. Hivyo mtu huyu atakuwa na upungufu wa damu wa kudumu. Mtu wa kawaida damu yake hb ni 11 hadi 17 lakini kwa hawa watu wanakuwa na damu mpaka 6 au 7 na huwa hazifanani wengine 8, 9 ,10 na wengine kawaida..kwa hiyo huwa tunawapa dawa za kuongeza damu kila siku kidonge kimoja cha folic acid.
Itaendelea
Dr.ibu 
Acha maoni ako hapo chini pia unaweza kutuma swali lako kupitia whatsap no 076757271 jina lako litakua siri kujiunga na group la whatsap bonyeza hapo https://chat.whatsapp.com/3fsRnLDkTZIFMqasAjJXWU Be healthy and happy

Swali:Nimetumia dawa za uzazi wa mpango damu inatoka haikatiki nini shida?

 Mgonjwa: Habari za uxubuhi my dr mwanamke ametumia dawa za family plan bt tangu achome damu haikatiki nn solution ya hapo
 Dr.ibu: Dawa za family planing zipo za njia tofauti... vidonge, za kuchoma, vipandikizi na loop au kitanzi,  n.k ... katika pia zipo njia za kutumia za kutumia kila tendo mf.condom zipo za kutumia kila siku mf.vidonge zipo za baada ya muda fulani... mf. Za kuchoma kila baada ya miezi mitatu, kipandikizi kila baada ya miaka mitano na loop kila baada ya miaka mitano na nyingine miaka 10... na emergency kama p2 na p1
Uzazi wa mpango ni bure..

Madhara yake zilizonyingi zinaleta kitu tunaita unscheduled bleeding yaani unatoa damu bila ratiba maalum... hali hiyo huwa inatokana na ile hali ya hormone ulizoingiza kupitia zile dawa ulizotumia... mara nyingi huwatokea watu ambao ni mara ya kwanza kutumia na pia hutokea siku za mwanzo baada ya kutumia njia fulani ya uzazi wa mpango... utokaji huu wa damu hupungua jinsi siku zinavyozidi kwenda na baadae huacha kabisa.. tafiti zinaonesha karibia utokaji damu unaotokana na njia zote za uzazi wa mpango unapungua au kutibiwa na hormone ya estrogen.. kwahiyo ukipewa estrogen hormon zote zinakaa sawa mwilini na hivyo damu inaacha kutoka.
Sasa kuna dawa gani yenye estrogen... hii ni homoni ambayo wataalamu wameiweka kwenye vidonge na wanatumia trade name au majina ya bidhaa mbalimbali  lakini ukienda pharmacy mwambie unaomba estradiol itakusaidia

Acha maoni ako hapo chini pia unaweza kutuma swali lako kupitia whatsap no 076757271 jina lako litakua siri kujiunga na group la whatsap bonyeza hapo https://chat.whatsapp.com/3fsRnLDkTZIFMqasAjJXWU Be healthy and happy

Nina ujauzito na tumbo linauma chini ya kitovu..

Swali.Nina ujauzito wa mwez mmoj na nusu lakn tumb linauma afu nakosa hamu ya kula
JIBu: Leo naomba tuelewane ujauzito huleta upungufu kidogo wa kinga mwilini ili mtoto aweze kukaa tumboni kwa sababu la sivyo kinga ya mwili itaua mtoto... kwa sababu mtoto aliyepo tumboni huwa anakuwa kama kitu au kiumbe kigeni ambacho hakikutakiwa kuwepo.. hivyo kinga ya mwili inapopungua unakuwa katika hatari ya kupata magonjwa tofauti na mtu wa kawaida.. na ukipata ugonjwa utakuwa wa nguvu zaidi na dalili zake zinakuwa kali zaidi kuliko ambaye hana ujauzito... magonjwa ambayo yanawashambulia sana ni UTI na malaria.. ndio maana tunashauri utumie dawa za malaria Sp na ulale kwenye NET kila siku.. lakini kwako nadhani utakuwa na UTI ambayo dalili zake ni..

1. Kuumwa tumbo hasa chini ya kitovu
2.homa na mwili kuchoka
3.kichwa kuuma na wakati mwingine kukosa hamu ya kula
4.maumivu unapokojoa
5.kukojoa mara kwa mara


Kwa mjamzito inatia changamoto kwa  sababu anakojoa mara kwa mara kawaida kwa sababu ni mjamzito lakini pia akikosa hamu ya kula,homa, na kichwa kuuma inaweza kuwa malaria na kwa sababu hajaanza dozi ya dawa za kuzuia malaria.
 Kujua ni kutumia kipimo kupima malaria na UTI kujua nani anakusumbua japo kwa sababu tumbo linauma more likely utakuwa na UTI maabukizi kwenye njia ya mkojo.

Acha maoni ako hapo chini pia unaweza kutuma swali lako kupitia whatsap no 0767357271 jina lako litakua siri kujiunga na group la whatsap bonyeza hapo https://chat.whatsapp.com/3fsRnLDkTZIFMqasAjJXWU Be healthy and happy

Saturday, 6 October 2018

KANSA YA MATITI

Wiki ya kansa ya matiti duniani...

Kansa ya matiti ni kati ya kansa au saratani ambazo zipo juu katika kuathiri afya ya wanawake duniani..kwa Tanzania ni ya pili ikitanguliwa na kansa ya shingo ya kizazi.

Hii huanza kama uvimbe ambao huwa hauonekani bali mtu anaweza kuuhisi akiwa anaoga au kujigusa au wakati mwingine mtu mwingine anaweza kuuhisi akiwa anagusa titi lake..
Hukua haraka na huweza kusababisha titi kuvimba, kubadilika rangi, baadae ngozi yake kuwa kama ganda la chungwa..lakini pia huweza kutokea kidonda ambacho hakina maumivu au unaweza kushangaa titi halichezi linakuwa linashikana  na kifua hata ukiinama halichezi... baadae mtu huweza kuwa na mitoki ikiwa kwapani ikivimba au kuwa na vidonda.. baadae kansa hii huweza kusambaa sehemu mbalimbali mwilini ikiwepo mifupa hasa ya mgongoni mtu anakuwa na maumivu ya mgongo na kiuno na wakati mwingine kuvunjika hata akidondoka kidogo tu.. kwenye ubongo ambapo mtu huwa anaweza kuwa kama na kifafa, kichwa kuuma sana hasa asubuhi na pengine kupoteza fahamu na kupoteza kumbukumbu...kwenye mapafu anakuwa anashindwa kupumua vizuri, kokohoa damu, na kifua kubana au kuuma... pia tumbo linaweza kujaa maji na kuvimba sana..

Saratani hii kama kansa nyingine chanzo hasa hakijulikani isipokuwa kuna vihatarishi ambavyo mtu akiwa navyo basi anaweza kuwa kwenye hatari ya kupata kansa ya matiti

1.sigara na pombe
2.uzito mkubwa
3.kama mtu kwenye familia aliwahi kuwa ugonjwa huu..wengine pia wanakuwa kwenye hatari... na kama alikuwa na kansa kwenye matiti yote mawili hatari inaongezeka pia kama aliipata akiwa na umri wa chini ya miaka 50 hatari inakuwa kubwa zaidi
4.utoaji wa mimba.. pia mimba inavozidi kuwa na miezi mingi ikitolewa au ikitoka hatari inazidi kuongezeka
5.kama ulishawahi kupata kansa hii unakuwa katika hatari ya kupata tena mara ya pili hata ukipona.
6.kuwa na uvimbe wowote kwenye ziwa kunakuweka katika hatari ya kupata kansa ya ziwa
7.kutokuwa na mtoto mpaka miaka 35 ndio maana zamani ulikuwa unajulikana kama ugonjwa wa masister
8.kuvunja ungo mapema kabla ya miaka 12
9.kuwa na watoto wachache kama mmoja pia ni hatari
10.kutumia dawa za homoni kwa wazee

NINI CHA KUFANYA
1.kagua matiti yako mara kwa mara unapooga
2.acha uvutaji wa sigara pia usikae na wavuta sigara,punguza uzito kwa kufanya mazoezi na punguza unywaji wa pombe
3.kama una ndugu alishawahi kuwa na ugonjwa huu fanya kipimo mamogram mara kwa mara angalau mara moja kwa miezi sita mpaka mwaka mmoja
4.ukihisi uvimbe ambao sio wa kawaida uwahi hospital haraka ukachunguzwe zaidi kumbuka inatibika ukiwahi.

Itaendelea
@dr.ibu
Acha maoni ako hapo chini pia unaweza kutuma swali lako kupitia whatsap no 076757271 jina lako litakua siri kujiunga na group la whatsap bonyeza hapo https://chat.whatsapp.com/3fsRnLDkTZIFMqasAjJXWU Be healthy and happy

Sunday, 23 September 2018

UVIMBE KWENYE KIZAZI. FIBROID


Imeandikwa na dr.Ibu


Mazoea ni kwamba mtu akisema kizazi anamaanisha uterus..

Hii ndio mara kwa mara mnasikia mkipigwa utrasound huko wanakuambia una uvimbe kwenye kizazi. Watu wengi wakasema nizungumzie.

Sasa huu ni moja ya aina ya uvimbe ambao unakuwa kwenye kuta za kizazi/Uterus. Ni uvimbe ambao ndio unaongoza kati ya aina zote za uvimbe kwenye kuta za kizazi. Mungu mkubwa uvimbe huu sio kansa na uwezekano wa kuwa kansa ni mdogo sana ni chini ya 0.1% maana yake ni mtu mmoja kati ya watu wenye uvimbe 1000.

Inakadiriwa kwamba 20% ya wanawake wakifika umri wa miaka 30 basi wanakuwa wameshapata fibroid. Uzuri ni kuwa asilimia kubwa 50% huwa hawana dalili yoyote wako freshi tu na hauwasumbui hata kidogo.
Na uvimbe huu huwapata zaidi watu :

1.weusi kuliko wenzetu wa rangi nyeupe.
2.watu ambao hawana watoto au wenye ugumba wa mtoto mmoja. Maana yake ana mtoto mmoja lakini anajaribu kupata ujauzito tena hawapati.

3.umri ambao wanakuwa wengi wanapata ugonjwa huu ni miaka kati yaa 35 na 45.
4.urithi kifamilia kama kuna mtu ana uvimbe na wanawake wengine kwenye familia kuna uwezekano wa kuwa na uvimbe japo sio lazima.

Ukuaji wa uvimbe huu hutegemea homoni ya estrogeni.. ndio maana

1.Huwa unaongezeka kwa watu ambao bado wanaona siku zao wakishaacha kwenye miaka ya 50 unapungua na baadae unaweza kupotea kwa sababu estrogen inakuwa imepungua sana mwilini

2.unaongezeka zaidi kipindi cha ujauzito kwa sababu homoni inakuwa nyingi kwenye mwili.

3.Haiwezi kutokea kabla ya kubalehe/ Kuvunja ungo kwa sababu homoni pia zinakuwa kidogo.

4. Baada ya kuacha siku zake mwanamke hawezi kuota fibroid mpya na zilizokuwepo zinapungua au kupotea kabisa kwa kunyauka.

5.inawapata watu wanene zaidi kwa sababu mafuta huwa yanaweza kutengeneza hizo homoni kwenye mwili.
6. Watu wanaotumia dawa za uzazi wa mpango zenye homoni moja.Ila hizo ambazo mnatumia sana siku hizi hazina uhusiano na fibroid.

Fibroid inaweza ikawa moja au zaidi ya moja na ukuaji wake huwa hauwi sawa nyingine inaweza kukua haraka kuliko nyingine.

Uvimbe huu chanzo chake kamili hakijulikani kisayansi.  Lakini kuna mawazo ya wanasayansi wengi wakisema unatokana na misuli ya kuta za uzazi kubadilika na kukua haraka zaidi ya kawaida na mwili kushindwa kuukontrol..
 Kwa hiyo mgonjwa anakuja hospital anaweza kuwa na mtoto mmoja mkubwa kuanzia miaka 10 nakuendela au hana mtoto kabisa...
Japo wakati mwingine wengine wanaweza wakawa na watoto wengi lakink kama amezaa akiwa na umri mdogo na akazaa mara kwa mara anaweza akawa kwenye kundi hili hatarishi kupata fibroid...umri wa kati ya miaka 35 hadi 45.

Dalili za  fibroid
Kama nilivosema zaidi ya 75% hazina dalili basi hugundulika kwa bahati tu kama hivo ukipiga utrasound au dr akiwa anagusa tumbo akaona kuna uvimbe.
Lakini kama dalili mara nyingi hutegemeana na ukubwa na sehemu ilipo.

1.kutoka damu nyingi ya hedhina inayoendelea kuzidi kila mzunguko. Hii ni kwa sababu inazuia kujiminya kwa mishipa ya damu ya kwenye kuta za kizazi ili damu isitoke.

2.mzunguko kuwa hautabiliki...kwenda hedhi mara nyingi zaidi ya kawaida.

3.maumivu wakati wa hedhi
4.maumivu wakati wa tendo
5.kushindwa kupata mimba
6.kupoteza mimba mara kwa mara kwasababu nafasi imejaa uvimbe kwahiyo mimba zinatoka
7.tumbo kuuma chini ya kitovu
8.kuvimba chini ya kitovu



Mchoro kuonesha aina mbalimbali za fiboid kutokana na eneo zilipo




Wednesday, 19 September 2018

SWALI:Doctor samahani naomba kuuliza swali. ninapokuwa natoa haja kubwa mgongo/kinyama kinatoka,sipati mauivu yoyote ila lazima nikirudishe kwa kidole naomba kujua nini hiki na kama kina athari kiafya

JIBU
Ugonjwa wako unaitwa bawasiri
Bawasili au hemorrhoids kitaalamu

Ni ugonjwa ambao hutokana na kuvimba kwa mishipa ya damu ambayo ipo sehemu ya chini ya njia ya haja kubwa(mkundu)

 Mishipa hii huvimba taaratibu na damu yake huweza aidha kuganda( thrombosed) au kuathiriwa na wadudu ( infected) na hapo ndio huwa na maumivu lakini la sivyo huwa haiumi.

Bawasiri zimegawanyika makundi mawili zipo ambazo hukaa ndani kabisa (internal hemorrhoids) na nyingine huwa zinakuwa nje na kwa juu zinakuwa zimevikwa ngozi ya kawaida pale kwenye mlango wa kuingilia (external hemorrhoids )...

NINI HUSABABISHA.
sababu kubwa ya kupata bawasiri ni hali ya wima ya binadamu tuliyonayo ambayo inasababisha damu inayoenda eneo la chini ya mwili kama miguu kutokana kushindwa kupanda juu kirahisi hii ndio sababu wanyama kama mbuzi, mbwa ambao hawapo wima hawapati hemorrhoids, damu isipopanda haraka inasababisha mishipa ile kutanuka na kuvimba na ndio tunaita hemorrhoids.

2. Kupata choo kikavu/ kigumu sana kutokana na kutokunya maji ya kutosha na vyakula vyenye nyuzi kama mboga za majani na matunda. Hii husababisha kubanwa kwa mishipa ya damu na kuzuia damu kupanda juu kurudi kwenye moyo na hivyo huleta uvimbe...

3. Kuwa na pressure kubwa tumboni...

Hii huzuia pia damu kurudi juu kwenda kwenye moyo kirahisi..hii huwapata watu  wenye uvimbe tumboni, au wajawazito, wanaofanya mazoezi ya kunyanyua vitu vizito na hao wenye constipation( choo kigumu) pia wazee wenye tezi dume au kansa ya kibovu cha mkojo

Zipo sababu nyingi lakini hizo ndio ambazo ni muhimu sana kwenu.


Dalili zake .
1. Kuhisi kuna kitu kipo ndani ya sehemu ya haja kubwa ambacho hakitoki
 Hisia hii huwa inategemeana na ukubwa wa uvimbe.
2. Huweza kutoka damu wakati wa kutoa haja kubwa
3. Maumivu wakati wa kutoa haja kubwa.
4. Kuhisi kuna kitu kinatoka na kurudi wakati wa kutoa haja kubwa.
5.kuona kabisa uvimbe umetokezea kwenye njia ya haja kubwa.

NB:uvimbe unaweza ukawa mmoja au zaidi ya mmoja. Mara nyingi hukaa sehemu kama ni saa ni sehemu ya saa 4, 7 na 11.

GRADE ZAKE..
1. Kunakuwa na uvimbe mdogo kwa ndani
2.uvimbe unakuwa unaweza kutoka nje mtu akijikamua tumbo na kurudi wenyewe akiacha kujikamua
3.uvimbe unakuwa unatoka mtu akijikamua na unaweza kurudishwa kwa kitu choxhote kama kidole na ikawezekana kukaa ndani

Grade 4. Unakuwa umetoka nje na hauwezi hata kurudishika ndani

MATIBABU NA NJIA ZA KUJIKINGA
 Matibabu yanategemeana na grade ya bawasiri.

Grade 1. Kuna dawa ambayo huwa tunachoma ambayo inakausha kabisa
Grade 2. Kuna ruber band wanaifunga kwa sehemu inapoanzia uvimbe(shina lake) alafu uvimbe wote unakauka kwa sababu unakosa damu

Au kuna kifaa kinaitwa stapler kinatumika kukata bawasiri mojamoja.

Grade 4 tunafanya operation  na kuna aina nyingi za operation.

Namna ya kujikinga.

1.kunywa maji ya kutosha
2.kula vyakula vya nyuzi nyuzi
3. Acha kunyanyua vyuma fanya mazoezi ya kawaida
4.fanya mazoezi kupunguza mwili
5. Usikae sana chooni.. kupokea simu au kusoma gazeti au kuchati chooni

6.tibu haraka kama una choo kigumu

7. Acha kujikamua wakati wa kukojoa au kutoa haja kubwa.

8. Ukijisikia haja kubwa usiibane nenda.
By @dr.ibu

SWALI:Nina shida naomba unisaidie..... Nilikua mjamzito early pregnancy ila jumatatu iliyopita nilifanya kaz ngumu ucku wake nkatokwa na dam nying sana nlienda hospital nkaambiwa mimba imetoka nlioshwa nkapewa dawa pamoja na sindano.... Dam ilikata kwa mda ila juz nliumwa sana na kutokwa na dam upya ila ikakata leo hali ileile imenirudia naomba nisaidie



 JIBU: Pole sana mom/dada... damu haitakiwi kuendelea kutoka ukiwa umeshasafishwa... uwezekano ni vitu viwili ni aidha  ilibakia hawakumaliza kitu ambacho uwezekano ni mdogo kama ikifanyika hospitali au kuna ugonjwa unaitwa   GTD (  Gestational Trophobastic Disease) ambao unaendelea kuwa na dalili za ujauzito hata kama mimba imeshatoka. Na ukipima mkojo kipimo cha mimba kinakuwa positive.   Kawaida mimba ikishatoka baada ya siku 14 kipimo cha ujauzito kile cha mkojo kinatakiwa kuwa negative lakini kwa hawa bado kinakuwa positive..


Chakufanya nakushauri nenda hospitali ya karibu kubwa ya wilaya, au mkoa au rufaa kaonane na daktari.. Utapigwa utrasound ambayo itaonesha vyote kama bado kuna mabaki ya mimba au huo ugonjwa wa GTD na pia utaangaliwa kama una upungufu wa damu na kama umepata maambukizi (infection) yoyote kwa kupima damu yako.  Alafu baada ya siku 14 kuisha unaweza kupima kipimo cha ujauzito kama nilivoeleza pale juu.  Pole sana mungu akusimamie upone. Alafu pia mimba ikitoka ni rahisi sana kupata mimba nyingine haraka sana kwa hiyo tunashauri watumie njia za uzazi wa mpango... na njia nzuri kwao ni loop ambayo unaweza kutoa na ukapata mimba muda wowote bila kusubiri kama sindano




Tuesday, 18 September 2018

SWALI: Doctor samahani naomba kuuliza swali, nina mtoto binti wa shule nimemkuta na miso chumbani kwake je dawa hiyo ina kazi gani?

Miso kama jina maarufu ndugu alivouliza hiko ni kifupi tu ila inaitwa misoprostol...ni dawa inayotumika zaidi kuongeza contraction ( kujikunja kwa kuta za  mji wa uzazi) na ndio maana wengine wanazitumia katika kutoa mimba... pia hospital tunatumia kusafishia kizazi au kutoa mimba ambayo imefia tumboni... pia tunaitumia kuzuia damu kutoka kama mama katoa damu nyingi sana baada ya kujifungua na hayo yote yana dose tofauti... kuna namna tofauti na maarufu ni ile ya kuweka kwenye kuta za uke lakini ipo ya kumeza pia.

Ushauri ni kwamba ni kwamba kapime kama wanao ni mjamzito basi anawweza akawa alikuwa anataka kuitoa mimba. Pia ongea nae taratibu madhara  ya kutoa mimba na  kutumia dawa bila kuandikiwa na daktari


Acha maoni ako hapo chini pia unaweza kutuma swali lako kupitia whatsap no 076757271 jina lako litakua siri

kujiunga na group la whatsap bonyeza hapo  https://chat.whatsapp.com/3fsRnLDkTZIFMqasAjJXWU


Be healthy and happy

Dr.ibu

SWALI:Doctor samahan mama angu anatatizo limesumbua kwa mrefu , anadai kila akila chakula na akinywa maji, maji hayo yanaenda kubana sehemu ya juu upande wa kushoto na wa tumbo mauvivu makali sana anayapata. tatizo lake ni nini?


 Ila nadhani anacho maanisha ni kwamba akila chakula anapata maumivu yanayokuwa makali yanakuwa kama yanaunguza na yanazunguka mgongoni pande zote .

Hii ni aina ya maumivu yanayotokana na vidonda vya tumbo...

Watu kama hawa huwa inafika kipindi hawagusi chakula kabisa kwa sababu ya maumivu...aina hii ya vidonda vinakuwa kwenye mfuko wa tumbo kabisa ( stomach ulcer). Hawa huwa wanakonda sana kutokana na kuacha kula sababu ya maumivu


Aina nyingine ya vidonda vya tumbo( PUD) hizi hukaa kwenye utumbo mdogo (duodenal ulcer) hizi huuma wakati wa njaa hivyo watu kama hawa huwa hawavumilii njaa. Wakati mwingine wanaamka kabisa usiku kutafuta chakula au kupika hata saa nane usiku wanakula sana na wananenepa kupindukia.

Dawa zao ni zilezile dawa tatu  antibiotic mbili na moja kwa ajili ya kuzuia asidi amoxicillin pantoprazole na metronidazole anakunywa kwa siku 14 au ananunua kuna package  ipo na zote inaitwa heligokit.



Acha maoni ako hapo chini pia unaweza kutuma swali lako kupitia whatsap no 076757271 jina lako litakua siri

kujiunga na group la whatsap bonyeza hapo  https://chat.whatsapp.com/3fsRnLDkTZIFMqasAjJXWU


Be healthy and happy

Dr.ibu





Monday, 17 September 2018

SWALI .Dr habar,samahan mm ni mjamzto wa miez mi3 sasa lakn pia nilianza bleed tarh 6 nkamalza tarh8 nkaenda kukutana na mpnz wa tarh 12-21ndpo nkaondoka jion lakn baada ya kuondoka skuondoka nilienda tena kukutana na mchepuko wang tarh 22 usku alikuwa anatoa nje pia nkakutana naye tena tarh 28 usku.mzunguko wangu ni a siku 28. plz naomba kujua hii mmba itakuwa ya yule wa kwanza au wapl plz naomba nijbu

JIBU
kwanza kabisa pole kwa msongo mawazo ambao upo nao kwa sasa.

Ukitaka kujua baba a mtoto unataakiwa kujua siku zako za hatari za kutungishwa mimba katika mzunguko wako. Katika mzunguko wa kila mwanamke kuna sehemu mbili(2 phases).

Sehemu ya folicular ambayo ni sehemu ambapo yai linapitia mabadiliko mbalimbali ili liweze kurutubishwa. Katika hatua hii pia kunakuwa na maandalizi ya kuta za mji a uzazi (uterus) ka ajili ya mimba kutunga na kutunzwa kwa miezi tisa (wiki 36 hadi 40). Phase a folicular haina idadi kamili ya siku ila huanza siku ya kwanza mwanamke anapoanza mzunguko wake (siku ya kwanza ya hedhi) hadi siku yai linapotoka kwenye ovari (ovulation day). siku hii hutofautiana kutokana na urefu wa mzunguko wa mwanamke husika.

sehemu ya luteal
Au kitaalamu luteal phase hii huwa ni sawa  kwa kila mwanamke. ni idadi a siku ambazo yai linaweza kuishi, hii huchukua siku 14 tu.

Kitu kingine cha msingi kujua ni kwamba mbegu ya kiume huweza kuishi kwa siku 2-3 (masaa 48-72) hivyo ukijamiiana siku tatu kabla ya yai kutoka litaikuta mbegu ya kiume na kuna uwezekano wa kurutubishwa na ukapata mimba.
Pia yai likishatoka kwenye ovari hukaa siku mbili mpaka tatu ndio hapo ukuta wake hua mgumu na mbegu haiwezi kutoboa ili kurutubisha. kwahiyo mtu akifanya mapenzi ndani ya muda huo ndio urutubishwaji hutokea


Mzunguko wa mwanamke unatofautiana ila wa kawaida ni kuanzia siku 21 hadi 35 hivyo basi hata siku zao za yai kutoka zinatofautiana isipokuwa tu luteal phase ambayo ni siku 14 hazibadiliki

ukitaka kujua siku ya yai kutoka unachukua idadi ya siku katika mzunguko unatoa 14 abazzo ni siku ambazo yai linaweza kuishi.

kwa swali la dada itakua 32-14 itakuwa 18. Kwahiyo siku yake ya yai kutoka inakuwa siku ya 18, ukiangalia tarehe tokea tarehe 6 siku 18 ni tarehe 23.  kumbuka yai linakaa siku tatu na shahawa zinakaa siku 3 kwa hiyo kila aliyefanya naye mapenzi siku tatu nyuma au mbele ya tarehe 23 ni muhusika.Kwahiyo kuanzia wa tarehe 20 hadi 26 wote wamo katika siku hatari.

Boyfriend alikuwa naye tarehe 20 na tarehe 21 ni siku hatari na akachepuka tarehe 22 ambayo ni siku hatari zaidi.

Lakini ukitumia sayansi kwamba jinsi siku zinavozidi kwenda mbegu ya kiume hua inazidi kupoteza nguvu wa tarehe 22 anakuwa na uwezekano mkubwa zaidi kwa sababu mbegu zake zilikaa siku moja tu ndio yai likafika.

Hata ukiongeza na kwamba alikua anamwaga nje bado yeye ndio kuna uwezekano kubwa zaidi kwa sababu njia hii huwa sio effective sana. uwezekano wake wa kuzuia ujauzito ni chini ya 30%

Jibu kamili ni DNA.

Acha maoni ako hapo chini pia unaweza kutuma swali lako kupitia whatsap no 076757271 jina lako litakua siri

kujiunga na group la whatsap bonyeza hapo  https://chat.whatsapp.com/3fsRnLDkTZIFMqasAjJXWU


Be healthy and happy

Dr.ibu






Swali: Kuna dawa za kuzuia mimba zinaitwa P2 je hizo dawa ukiwa unatumia Mara kwa Mara huwa zina madhara yeyote kwenye mwili


JIBU:

P2 ni jina limezoeleka la dawa za kuzuia ujauzito kama mtu kafanya mapenzi katika siku za hatari.... ni njia ambayo inatumika sana lakini watu wengi hawaulizi matumizi yake au wanapuuzia matumizi kadri yanavotakiwa ...

Ukweli ni kuwa p2 ni dawa ambayo inatengezwa na hormone. Na inafanya kazi kwa kuchelewesha yai lisitoke kwenye ovari au kuzuia mbegu za kiume zisiingie kwenye mji wa uzazi zipate taabu kusafiri kwa kuzalisha uteute mgumu utakaoipa shida shawahawa kusafiri na kurutubisha yai..

UNAMEZAJE??
ukiona umefanya mapenzi na ukahisi umefanya siku za hatari na hujapanga kupata mimba unatakiwa kumeza dawa hizo...dose ni vidonge viwili 150gm jumla ni either kumeza vyote viwili au unameza kimoja alafu unasubiri masaa 12 unameza kilichobaki au kumeza vyote viwili kwa pamoja.. ila ya kumeza vyote viwili ndio ina faida kubwa zaidi.

Lini unatakiwa kumeza dawa hizi?...

The earlier the better wazungu wanasema wazungu.. dawa hizi zinakukinga mpaka kwa muda wa masaa 72 siku tatu. Unaruhusiwa kutumia ndani ya masaa 72 baada ya kufanya sex... baada ya hapo hazikusaidii.. ila uwezo wa kuzuia mimba unapungua jinsi siku zinavyozidi kusogea mbele mfano ukinywa kidonge cha kwanza ndani ha masaa 12 ya kwanza uwezo wa kuzuia ujauzito ni 95% ila ukinywa siku ya tatu baada ya masaa 48 ni 58% tu. Hivyo ni vizuri kuwahi..

Tahadhari
Hii sio njia ya uzazi wa mpango... ni vyema kutumia njia za uzazi wa mpango za kawaida kama mipira ili pia tujikinge na maradhi ya zinaa..

Pili hutakiwi kutumia njia hii zaidi ya mara moja kwa mwezi madhara yake unaharibu balance ya homoni na utableed sana na mzunguko wako utakuwa haueweki na pia unaweza pata machunusi usoni na ngozi kuwa na mafuta yaliyozidi.

Tatu ni gharama. Kwa dsm gharama yake inarange kuanzia 5000 mpaka 10000 hii ni kubwa sana ukizingatia bei ya kondomu au njia ya kudum ya uzazi wa mpango ambazo ni bure

"Be healthy and happy"

Nawapenda sana

Acha maoni ako hapo chini pia unaweza kutuma swal lako kupitia whatsap no 076757271 jinalako litakua siri

kujiunga na group la whatsap bonyeza hapo  https://chat.whatsapp.com/3fsRnLDkTZIFMqasAjJXWU


@dr.ibu

Mdogo wangu alitoboa masikio na sindano masikio yametoka uvimbe je dawa yake ni nin?

 JIBU
 la sikio kwanza nakushauri asitibu kienyeji sana aende hospital Kutibu hapo inategemeana na ukubwa wa uvimbe... kama ni mdogo sana atapewa antibiotics na za maumivu tu atapona kama ni mkubwa atapasuliwa utakamuliwa atapewa dawa za maumivu na antibiotics

 Lakini tujifunze nini imetokea kwenye sikio lake.....kwenye ngozi kuna wadudu wengi sana ikiwemo bacteria.... bacteria maarufu zaidi anayeishi kwenye ngozi ni staphylococcus aureus anaishi bila kusababisha shida yoyote kama (normal flora)mpaka akiingia kwenye sehemu nyingine ya mwili ndio husababisha shida huyu ndio husababisha majipu na miwasho na vipele vingi kwenye ngozi... sasa mtu ukijitoboa ngozi au kwa hapo kutoga masikio bila kusafisha lile eneo kwa dawa au spirit unampa uwezo wa kuingia kwenye sehemu ya ndani anayoweza kuleta madhara...ndio maana kabla ya upasuaji huwa tunasafisha ngozi yote kwa iodine ili kuua kwanza hawa wadudu.... na tunaosha mikono kwa dawa maalumu pamoja na kuvaa gloves maalumu kuzuia wadudu hawa wasilete madhara lakini pia tunaongeza na antibiotics za kutumia ili hata kama wameingia wafe na ile dawa
MAADA 1.

MZUNGUKO WA KAWAIDA WA MWANAMKE.

Unapozungumzia afya ya binadamu wa kike huwezi kuacha kitu muhimu kuliko vyote ambacho ni mzunguko wake wa hedhi. Je ipi ni kawaida na ipi si kawaida na je ni vitu gani vinasababisha isiwe kawaida na magonjwa ambayo huambatana na mzunguko wa hedhi usio wa kawaida.    Kwa kawaida binadamu wa kike hupata hedhi ya kwanza akiwa na umri wa miaka 13-17 lakini chini ya miaka 12 na baada ya miaka 17 ndio tunamuweka kwenye group la aidha kawahi mno au kachelewa kupata hedhi. Baada ya hapo huanza kupata hedhi kila baada ya siku 21 mpaka 35 ( utafiti mpya unasema kawaida ni siku 22-38 bado ni kawaida) na kila kwenye mzunguko anapata hedhi kwa siku 3-7 ( utafiti mpya hadi siku 8 ni kawaida na chini ya siku 2 inakuwa sio kawaida). Hivyo basi hali yoyote ambayo itakuwa kinyume na hapo inaweza kuwa inaambatana na magonjwa. Mzunguko huu hudhibitiwa na homoni za kike ambazo hutolewa na kudhibitiwa na ovari na ubongo.   
Matatizo ya hedhi ambayo yapo sana mazingira yetu ni kama ifuatavyo:

1. Maumivu wakati wa hedhi(dymenorrhea)

Maumivu wakati wa hedhi huwata wadada na wamama wengi. Tafiti nyingi zimefanyika kuhusu tatizo hili na inaonekana inatokana na vitu vingi ila mojawapo ni kuvutana kwa kuta za mji wa uzazi (uterus) na dalili zake ni maumivu ya tumbo,  mgongo na kiuno. Utafiti uliofanywa dar es salaam ulionesha wanafunzi asilimia 76 wa sekondari wanatatizo hili. Lakini habari njema ni kuwa asilimia kubwa ya watu maumivu huwa yanapungua kadri umri unavoongezeka. Na mpaka anapozaa mtoto wa kwanza asilimia kubwa maumivu huwa yanapotea kabisa.  Dawa yake ni kutumia dawa za maumivu kuanzia panadol, diclofenac, ikizidi sana huwa inakuwa imetokana na hormone zinakuwa zimezalishwa kwa wingi mno kwahiyo unapewa dawa za kubalanzi homoni ambazo ni vidonge vya uzazi wa mpango kwa siku 28 baada ya hapo unakuwa poa.

2. Kupata damu nyingi.

Hapa ni either kupata damu zaidi ya siku 8 au damu inatoka nyingi sana kwa siku mpaka mtu anakosa nguvu, kupoteza fahamu, kuumwa sana na kichwa kusikia mapigo ya moyo yanaenda mbio, kupata taabu kupumua na kwenda kuongezewa damu wakati mwingine. Na mara nyingi damu hutoka mfumo wa mabonge mabonge(clots).  Damu ya hedhi kawaida ni isizidi mills 80 ( chupa ya soda ina 350 mls).
Mara nyingi watu hawa huweza kupata damu katikati ya mzunguko maana yake kabla siku za kupata hedhi yake anapata katikati na siku zake zikifila tena anapata kama kawaida. Hii husababishwa na magonjwa mengi ikiwemo
Polyp-kwenye mji wa uzazi kuna kuwa na uvimbe ambao sio kansa

Fibroid-huu pia ni uvimbe lakini utofauti na polyp  ni kuwa poly inakuwa kama vidole na pia vinavyochomoza kwenda katikati ya uterus.